MAGARI YA CBT YAENDELEA NA KAZI YA UCHIMBAJI WA VISIMA KATIKA KONGANI YA VIWANDA MARANJE
Magari yaliyonunuliwa na Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) kwa ajili ya kusaidia shughuli za uchimbaji wa visima yanaendelea na kazi katika eneo la Kongani ya Viwanda Maranje, Nanyamba, Mkoani Mtwara. Magari hayo ni sehemu ya jitihada za CBT kuwezesha upatikanaji wa huduma muhimu za maji na kuharakisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika eneo hilo la kimkakati kwa maendeleo ya tasnia ya korosho. Uchimbaji wa visima katika Kongani ya Viwanda Maranje unalenga kuwezesha upatikanaji wa maji kwa ajili ya shughuli mbalimbali zinazotarajiwa kufanyika katika eneo hilo, ikiwemo shughuli za viwanda na huduma nyingine za msingi. Hatua hii inaendelea kuonesha dhamira ya CBT ya kuwezesha mazingira bora kwa ajili ya uwekezaji, uchakataji na uongezaji thamani wa korosho nchini.